Header Ads

Header Ads

HUMJUI MISS KK….? HUYU HAPA!! ANAZINDUA NGOMA YAKE’WANANUNA’!!


Na: Kione Hamis Mahuruku.
               Ukimtazama utapenda kumuangalia muda wote jinsi alivyo mcheshi,na zaidi hatokuboa kabisa,na ni Msela haswa kimuonekano.Ni Rapa mkali mwenye kujua nini anachokifanya,na anajua thamani ya Muziki aufanyao.Ni Latifa Mussa au kwa jina lake la kutafutia Mkate anajulikana zaidi kwa jina la Miss KK.Kwa wanaofuatilia Muziki wa Bongo Fleva kwa sasa si jina geni Machoni na Masikioni mwao.

                 Miss KK ana ujio mpya sasa,siku ya Jumamosi Tarehe 24/2/2018 atazindua Wimbo wake mpya kabisa.Wimbo unaoitwa ‘Wananuna’,atazindua Audio na Video.Uzinduzi huo utafanyika katika Hoteli ya Pallet maeneo ya Mbezi Beach.’Nimeona na mimi nifuate Nyayo za Watanzania wenzangu kuzindua  Audio na Video kwa pamoja,kule South Afrika huwa tunaanza kuachia Audio na baadae Video.Imebidi nikae na kuusoma Mchezo wa hapa Home pia’.Alisema Miss KK.

                 Amesema kwa sasa amebadili Menejimenti na atakuwa chini ya Kampuni ya KOI Entertainment na Meneja wake ni DJ Kinywele pamoja na usimamizi wa karibu kabisa kutoka kwa Kampuni ya WANENE ENT.Amesema pia,Show hiyo ya uzinduzi itaanza saa moja za jioni hadi usiku mkubwa.Watakaofika mapema saa moja hadi saa tatu usiku watapata Complimentary kwa na Vinywaji.Lakini watakaochelewa watachangia kiingilio cha Elfu Tano(5,000/-) kwa mtu mmoja.

                Miss KK anasema zaidi kwamba, ameshapata uzoefu mkubwa katika Muziki kwa sasa.Mwaka 2015 nilianza kwa kuachia Ngoma yangu iliyoitwa ‘Anginandaba’ ambao kwa Kiswahili unamaanisha ‘Sijali’ au kwa Kingereza ‘I don’t care’.Ngoma hiyo iliingia katika chati za  Radio ya Gagasi FM ya Durban na nikaitwa kwa mara ya kwanza katika Interview na kupata idadi kubwa ya Mashabiki.Alisema Miss KK.

                Baadae nikaachia Ngoma mfululizo ambazo ni Getting lit,Baridi tu na Kata Kiuno.Baadae Ngoma kufanya vizuri kule South Afrika,ndipo nikapata ushauri na Watu mbalimbali nikashauriwa nigeukie nyumbani Tanzania.Ndipo mwezi Disemba mwaka 2016 ikanilazimu nirudi Bongo na kuanza Mchakamcha wa kujitambulisha hapa nyumbani.Alhadullillah kwa sasa nimeanza kufahamika sana lakini hapo mwanzoni ilikuwa ngumu sana watu kunielea.Alieleza Miss KK.

              Kubwa Zaidi alisisitiza kwamba kutakuwa na Wasanii wengi watakaomsindikiza katika uzinduzi huo pamoja na Wasanii wanaomilikiwa na Kampuni ya WANENE ENT.Amesema kwa mtu atakayekwenda PALLET HOTEL,ukitokea Kawe unapita ilipo Radio TIMES FM mbele kidogo ukiuliza utafika.Ameomba Watu wajitokeze kwa wingi wakakate kiu ya Burudani.Kwa taarifa Zaidi pia fuatilia Clan TV Online.
             

No comments: